Maana ndefu ya Ishara ya msalaba
_Ishara ya msalaba ina maana ndefu sana!_
1. _Kukiri ukombozi wetu ulipatikana kwa Yesu Kristo kupitia msalaba_
2. _Kukiri utatu Mtakatifu yani Mungu Baba, Mungu Mwana na Mungu Roho Mtakatifu!_
3. _Tunaposhikanisha vidole vitatu wakati wa kufanya ishara ya msalaba, tunajiunganisha na Mungu katika nafsi tatu au tunapotumia vidole vyote vitano, tunakili madonda matano ya Yesu kristo!_
4. _Tunatumia mkono wa kulia kufanya ishara ya msalaba (unaomanisha mamlaka)_
5. _Tunapoanza kufanya ishara ya msalaba tunaanzia kwenye paji la uso kisha kifuani au kitovuni (ikimaanisha Mungu Baba alimtuma mwanaye kutoka juu mbinguni na kuja duniani)_
6. _Tunaelekea bega la mkono wa kushoto kisha kulia (hii inamaanisha Yule aliyetumwa kutoka mbinguni kuja duniani, alitutoa katika uovu (kushoto) na kutuleta katika wokovu (kulia)_
7. _Baada ya kukiri vyote hivyo tunafunga mikono ambayo dole gumba hupishana kwa kutengeneza namna ya msalaba! Kama ishara kuu iliyotumika katika kumnyanyua yule tunaemwabudu yaani (Kristo Yesu)_
_Na mwisho tunasema Amina tukimaanisha iwe hivyo (yaani tudumu katika ukombozi huo
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
0 comments:
Post a Comment